Sunday 29 October 2017

Federer amchapa Del Potro michuano ya Uswisi

Federer ameshinda vikombe saba mwaka 2017 ikiwemo Wimbledon na Australian Open
Mchezaji namba mbili kwa ubora katika tenisi duniani kwa upande wa wanaume Roger Federer amefanikiwa kumshinda Juan Martin Del Potro katika michuano ya ndani ya Uswisi.
Ameshinda kwa seti 6-7 (5-7) 6-4 6-3 huku akionyesha kiwango cha hali ya juu ikiwa ni wiki moja kabla ya michuano ya Paris Masters.
Ushindi huu unamfanya kupunguza pengo kati yake na mchezaji namba moja duniani Rafael Nadal.
Federer ameshinda taji lake la nane katika michuano hiyo ya Basel likiwa niu la saba kwa mwaka 2017.

Labels:

0 Comments:

Post a Comment

Subscribe to Post Comments [Atom]

<< Home