Monday 6 November 2017

Trump: Japan itayatungua makombora ya Korea Kaskazini



Bwa. Trump na mwenyeji wake Shinzo Abe, katika ziara yake ya kwanza nchini Japan na Bara Asia kama Rais wa MarekaniRais wa Marekani Donald Trump, amesema kwamba Japan itatungua makombora ya Korea Kaskazini, kwa kutumia mitambo ya kijeshi iliyonunuliwa kutoka Marekani.
Wakati huo huo, waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe, amesema kwamba, taifa lake litatungua makombora hayo kabla ya kutua ardhini, "ikiwa hilo litahitajika".
Viongozi hao wawili, walisema hayo walipozungumza na waandishi habari wakati wa kumalizika rasmi kwa ziara ya kwanza ya kitaifa ya Bwana Trump nchini Japan.
Katika miezi ya hivi karibuni, Korea Kaskazini imerusha makombora mawili hatari juu ya mipaka ya Japan.
Trump aapa kukabiliana na Korea Kaskazini kwenye ziara yake ya Bara Asia.
Alipokuwa akijibu maswali ya waandishi habari leo Jumatatu, Bw Trump alisema kwamba, Bwana Abe atanunua "kiasi kikubwa cha zana za kivita" kutoka Marekani.
Akigusia zana hatari za kinuklea za Korea Kaskazini, Trump alisema kuwa Bw Abe "atazishambulia zikiwa bado angani" mara tu atakapokuwa amemaliza kununua silaha hizo za kijeshi, anazosema kuwa itatoa ajira ya kazi kwa Wamarekani na pia "kutoa usalama kwa Japan".
Kwa habari zaidi Bonyeza hapa: www.zakacheka.blogspot.com

Labels: , ,

Sunday 5 November 2017

MILIKI BLOG YAKO MWENYEWE KWA TSH 40,000/=



NINATENGENEZA BLOG KWA TSH 40,000/= WASILIANA NAMI KWA 0625966236 / 0758590489
PIA NATENGENEZA APP KWA TSH 100,000/=

Labels: , , ,

Sunday 29 October 2017

Mamia ya wafuasi wa IS wakamatwa Uturuki

Polisi wa Uturuki wakiwa katika mazishi ya mmoja wa polisi mwenzo aliyeuawa na IS mwezi AgostiPolisi nchini Uturuki imewakamata mamia ya watu wanaodhaniwa kuwa wafuasi wa kikundi cha wanamgambo wa IS.
Raia wawili wa Azerbaijan na wengine 28 wa Syria, ni miongoni mwa waliokamatwa katika mji wa Mashariki wa Erzurum na mji wa Bursa uliopo Kaskazini Magharibi.
Wengine walikamatwa katika mji mkuu Ankara siku ya Jumamosi.
Mpiganaji wa IS aliwaua watu 39 katika ukumbi mmoja wa usiku uitwao Reina mjini Istanbul, na tukio hilo bado limeacha simanzi kubwa.

Labels:

Kampuni zashindania kukuza bangi Denmark


BangiHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Kampuni nchini Denmark zimeanza kuwasilisha maombi kwa serikali kupata idhini ya kukuza bangi kujiandaa kwa wakati ambao bangi itakuwa halali nchini humo mwaka ujao.
Kampuni 13 tayari zimewasilisha maombi kwa idara ya serikali inayohusika ya Laegemiddelstyrelsen.
Bangi itakuwa halali kutumiwa kama dawa na watu wanaotatizwa na magonjwa yenye uchungu mwingi kama vile saratani na kuganda kwa misuli.
Kuanzia Januari 2018, bangi itakuwa inatolewa kama dawa kwa wagonjwa kwa majaribio ya kipindi cha miaka minne.
Gazeti la Copenhagen Post linasema kuanzia wakati huo, wagonjwa wanaweza kupendekezewa bangi kama dawa na daktari nchini humo.
Lakini bunge bado linajadiliana kuhusu mfumo utakaotumiwa.
Hilo limezifanya kampuni kubwa za kilimo cha mboga na matunda nchini humo kama vile Dansk Gartneri ya Jorgen K. Andersen kutowasilisha maombi kwa sasa.
Bw Andersen ameambia tovuti ya fyens.dk kwamba kampuni yake inatazamia kwamba kutakuwa na mkanganyiko mkubwa katika kutolewa kwa idhini ya kukuza bangi.

Labels:

USHIKAMANA NA MAKAHABA CHANZO CHA UMASKINI part 02

Mpendwa msomaji, Ninafuraha kuu kukutana nawe tena siku hii ya leo tukiendelea sehemu ya pili ya somo letu.Ni mimi Ev. Zachary John Bequeker - Mwanza Tanzania.


Tulijifunza juu ya ukahaba. Tukaangalia maana ya ukahaba, Maana ya kahaba, Namna ukahaba unavyofanyika, Mavazi ya kikahaba na Madhara yake.

Kama hujafanikiwa kusoma sehemu ya kwanza ya somo hili bonyeza hapa chini

Tunasoma katika kitabu cha MITHALI 29:3 "Apendaye hekima humfurahisha babaye; Bali ashikamanaye na makahaba hutapanya mali."


Kushikamana na makahaba ni kitendo cha kuwa nao na kuutumia muda kwa pamoja"A Companion of harlots"

Ni dhahiri kuwa, Unapotumia muda wako kuwa na kahaba kuna gharama zinazohitajika.
Inahitajika umuhudumie kwa chakula, ulipie chumba au gharama ya mahali pa kutumia muda wenu pamoja.

Jaribu kuwaza kwa mfano wewe una kipato cha Tsh. 300,000/= kwa mwezi, ambayo ni wastani wa Tsh 10,000/= kwa siku. Jiulize Je, Tsh 10,000/= inatosheleza kumhudumia kahaba,kulipia chumba na gharama zingine?  

Jibu ni la! Haiwezi kujitosheleza. Na matokeo yake ni nini? Matokeo yake itakuwa unahangaika kila siku kutafuta pesa, Pesa unapata lakini hautaona hatua zozote za maendeleo kwa sababu unachota maji na kuyatia ndani ya tenga.

Hata kama ungalikuwa unampatia Tsh 2,000/= kwa siku bado ni nyingi sana. Chukua 2000 x 30 = 60,000/= na ukizidisha kwa miezi 12 unapata ni 720,000/= 

Watu wengi walio rudi nyuma kimaendeleo chanzo ni makahaba. Uliza watakuambia na hata hivyo wewe mwenyewe ni shahidi wa jinsi makahaba wanavyokwamisha mipango yako au walivyokuwa wakikwamisha mipango yako.

Wakati mwingine kuna kuambukizwa magonjwa ya zinaa, badala ya kufanya shughuli za kimaendeleo unaanza kuhangaika kutafuta tiba ya magonjwa hayo. na tiba si bure! bali ni gharama zinahitajika ambazo ni pesa, muda n.k.

Hebu badilika sasa.Achana na tamaa za ukahaba.Hebu tosheka na mme au mke uliyenaye.
UTABADILI BUCHA LAKINI NYAMA NI ILEILE Ikimbie zinaa mara moja sasa 1 KOR 6:18
  Tumeambiwa "Mme mmoja,Mke mmoja" na si vinginevyo  1 KOR 7;2

Kama hujaoa wala kuolewa subiri muda ukifika uataoa au kuolewa. Mwombe Mungu atakupatia unayemhitaji kwani Mungu anakuuliza unataka nikufanyie nini? Mwambie Mungu nataka unipe mke au Mungu nataka unipe mume.

UKO TAYARI KUONDOLEWA KIU YA UKAHABA ?
Naamini uko tayari. Fuatisha maneno haya kwa dhati ya moyo wako na baada tu ya kumaliza uataona badiliko katika masha yako.

SEMA   " Mungu Baba, Mimi ni mchafu mbele zako, Nimekutenda dhambi kwa namna ya kutisha, Lakini sasa naja mbele zako nikihitaji msamaha. Nakuomba Bwana ufute jina langu katika vitabu vya hukumu na uliandike katika kitabu cha uzima wa milele. Mungu ondoa kiu ya ukahaba ndani yangu kuanzia sasa niwe mtoto wako. Sitaki ukahaba tena. Nipe roho ya kutosheka na mke/mme niliyenaye Katika jina la YESU AMEN!" 
Sasa umeokoka , hamu ya ukahaba haipo tena.

Tafuta mahali penye kanisa linalohubiri wokovu kwa msaada zaidi na Mungu akubariki.
WASILIANA NAMI KWA 0758 590 489/ 0625 966 236




Share on Google Plus

MSIMAMIZI WA BLOG HII

Mimi ni mwinjilisti Zachary John Bequeker toka Mwanza Tanzania. Karibuni tujifunze neno la Mungu pamoja.
pia waweza pata masomo ya neno la Mungu Youtube kwa kuandika Zachary Bequeker au ZAKACHEKA.
0625 966/ 0758 590489

Labels:

USHIKAMANA NA MAKAHABA CHANZO CHA UMASKINI part 02

Mpendwa msomaji, Ninafuraha kuu kukutana nawe tena siku hii ya leo tukiendelea sehemu ya pili ya somo letu.Ni mimi Ev. Zachary John Bequeker - Mwanza Tanzania.


Tulijifunza juu ya ukahaba. Tukaangalia maana ya ukahaba, Maana ya kahaba, Namna ukahaba unavyofanyika, Mavazi ya kikahaba na Madhara yake.

Kama hujafanikiwa kusoma sehemu ya kwanza ya somo hili bonyeza hapa chini

Tunasoma katika kitabu cha MITHALI 29:3 "Apendaye hekima humfurahisha babaye; Bali ashikamanaye na makahaba hutapanya mali."


Kushikamana na makahaba ni kitendo cha kuwa nao na kuutumia muda kwa pamoja"A Companion of harlots"

Ni dhahiri kuwa, Unapotumia muda wako kuwa na kahaba kuna gharama zinazohitajika.
Inahitajika umuhudumie kwa chakula, ulipie chumba au gharama ya mahali pa kutumia muda wenu pamoja.

Jaribu kuwaza kwa mfano wewe una kipato cha Tsh. 300,000/= kwa mwezi, ambayo ni wastani wa Tsh 10,000/= kwa siku. Jiulize Je, Tsh 10,000/= inatosheleza kumhudumia kahaba,kulipia chumba na gharama zingine?  

Jibu ni la! Haiwezi kujitosheleza. Na matokeo yake ni nini? Matokeo yake itakuwa unahangaika kila siku kutafuta pesa, Pesa unapata lakini hautaona hatua zozote za maendeleo kwa sababu unachota maji na kuyatia ndani ya tenga.

Hata kama ungalikuwa unampatia Tsh 2,000/= kwa siku bado ni nyingi sana. Chukua 2000 x 30 = 60,000/= na ukizidisha kwa miezi 12 unapata ni 720,000/= 

Watu wengi walio rudi nyuma kimaendeleo chanzo ni makahaba. Uliza watakuambia na hata hivyo wewe mwenyewe ni shahidi wa jinsi makahaba wanavyokwamisha mipango yako au walivyokuwa wakikwamisha mipango yako.

Wakati mwingine kuna kuambukizwa magonjwa ya zinaa, badala ya kufanya shughuli za kimaendeleo unaanza kuhangaika kutafuta tiba ya magonjwa hayo. na tiba si bure! bali ni gharama zinahitajika ambazo ni pesa, muda n.k.

Hebu badilika sasa.Achana na tamaa za ukahaba.Hebu tosheka na mme au mke uliyenaye.
UTABADILI BUCHA LAKINI NYAMA NI ILEILE Ikimbie zinaa mara moja sasa 1 KOR 6:18
  Tumeambiwa "Mme mmoja,Mke mmoja" na si vinginevyo  1 KOR 7;2

Kama hujaoa wala kuolewa subiri muda ukifika uataoa au kuolewa. Mwombe Mungu atakupatia unayemhitaji kwani Mungu anakuuliza unataka nikufanyie nini? Mwambie Mungu nataka unipe mke au Mungu nataka unipe mume.

UKO TAYARI KUONDOLEWA KIU YA UKAHABA ?
Naamini uko tayari. Fuatisha maneno haya kwa dhati ya moyo wako na baada tu ya kumaliza uataona badiliko katika masha yako.

SEMA   " Mungu Baba, Mimi ni mchafu mbele zako, Nimekutenda dhambi kwa namna ya kutisha, Lakini sasa naja mbele zako nikihitaji msamaha. Nakuomba Bwana ufute jina langu katika vitabu vya hukumu na uliandike katika kitabu cha uzima wa milele. Mungu ondoa kiu ya ukahaba ndani yangu kuanzia sasa niwe mtoto wako. Sitaki ukahaba tena. Nipe roho ya kutosheka na mke/mme niliyenaye Katika jina la YESU AMEN!" 
Sasa umeokoka , hamu ya ukahaba haipo tena.

Tafuta mahali penye kanisa linalohubiri wokovu kwa msaada zaidi na Mungu akubariki.
WASILIANA NAMI KWA 0758 590 489/ 0625 966 236




Share on Google Plus

MSIMAMIZI WA BLOG HII

Mimi ni mwinjilisti Zachary John Bequeker toka Mwanza Tanzania. Karibuni tujifunze neno la Mungu pamoja.
pia waweza pata masomo ya neno la Mungu Youtube kwa kuandika Zachary Bequeker au ZAKACHEKA.
0625 966/ 0758 590489

Labels: