Monday, 6 November 2017

Trump: Japan itayatungua makombora ya Korea Kaskazini



Bwa. Trump na mwenyeji wake Shinzo Abe, katika ziara yake ya kwanza nchini Japan na Bara Asia kama Rais wa MarekaniRais wa Marekani Donald Trump, amesema kwamba Japan itatungua makombora ya Korea Kaskazini, kwa kutumia mitambo ya kijeshi iliyonunuliwa kutoka Marekani.
Wakati huo huo, waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe, amesema kwamba, taifa lake litatungua makombora hayo kabla ya kutua ardhini, "ikiwa hilo litahitajika".
Viongozi hao wawili, walisema hayo walipozungumza na waandishi habari wakati wa kumalizika rasmi kwa ziara ya kwanza ya kitaifa ya Bwana Trump nchini Japan.
Katika miezi ya hivi karibuni, Korea Kaskazini imerusha makombora mawili hatari juu ya mipaka ya Japan.
Trump aapa kukabiliana na Korea Kaskazini kwenye ziara yake ya Bara Asia.
Alipokuwa akijibu maswali ya waandishi habari leo Jumatatu, Bw Trump alisema kwamba, Bwana Abe atanunua "kiasi kikubwa cha zana za kivita" kutoka Marekani.
Akigusia zana hatari za kinuklea za Korea Kaskazini, Trump alisema kuwa Bw Abe "atazishambulia zikiwa bado angani" mara tu atakapokuwa amemaliza kununua silaha hizo za kijeshi, anazosema kuwa itatoa ajira ya kazi kwa Wamarekani na pia "kutoa usalama kwa Japan".
Kwa habari zaidi Bonyeza hapa: www.zakacheka.blogspot.com

Labels: , ,

Sunday, 5 November 2017

MILIKI BLOG YAKO MWENYEWE KWA TSH 40,000/=



NINATENGENEZA BLOG KWA TSH 40,000/= WASILIANA NAMI KWA 0625966236 / 0758590489
PIA NATENGENEZA APP KWA TSH 100,000/=

Labels: , , ,

Sunday, 29 October 2017

Kampuni zashindania kukuza bangi Denmark


BangiHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Kampuni nchini Denmark zimeanza kuwasilisha maombi kwa serikali kupata idhini ya kukuza bangi kujiandaa kwa wakati ambao bangi itakuwa halali nchini humo mwaka ujao.
Kampuni 13 tayari zimewasilisha maombi kwa idara ya serikali inayohusika ya Laegemiddelstyrelsen.
Bangi itakuwa halali kutumiwa kama dawa na watu wanaotatizwa na magonjwa yenye uchungu mwingi kama vile saratani na kuganda kwa misuli.
Kuanzia Januari 2018, bangi itakuwa inatolewa kama dawa kwa wagonjwa kwa majaribio ya kipindi cha miaka minne.
Gazeti la Copenhagen Post linasema kuanzia wakati huo, wagonjwa wanaweza kupendekezewa bangi kama dawa na daktari nchini humo.
Lakini bunge bado linajadiliana kuhusu mfumo utakaotumiwa.
Hilo limezifanya kampuni kubwa za kilimo cha mboga na matunda nchini humo kama vile Dansk Gartneri ya Jorgen K. Andersen kutowasilisha maombi kwa sasa.
Bw Andersen ameambia tovuti ya fyens.dk kwamba kampuni yake inatazamia kwamba kutakuwa na mkanganyiko mkubwa katika kutolewa kwa idhini ya kukuza bangi.

Labels:

Je wajua kuna mipira ya kondomu ya mdomoni?


Umuhimu wa kutumia kondomu za mdomoni
Image captionUmuhimu wa kutumia kondomu za mdomoni

Nilipokuwa na umri wa miaka 20 shirika moja la wahisani walileta boksi la mipira ya kondomu katika chuo chetu.
Zilisambazwa miongoni mwetu kama maelezo ya kujikinga kiafya, huku tukipigwa na butwaa.
''Wakati ilipofika kwangu nilichukua pakiti moja. Ilikuwa mara yangu ya kwanza kukumbana na mipira ya kondmu ya mdomoni''.
Njia pekee ya kufikiria kuhusu 'dental dams' ni kuzichukulia kama kondomu za mdomoni.
Zina umbo la mraba na nyengine la mstalili na huwekwa katika uke ama sehemu ya nyuma kwa lengo la kufanya ngono ya kutumia mdomo bila kupitisha maambukizi.
Mara tu mipira hiyo inapowekwa katika maeneo yanayofaa unaweza kuendelea na shughhuli yako huku mipira hiyo ikiwa na ladha tofauti.
Haionekani kuwa mizuri lakini inazuia maambukizi.
Nchini Uingereza , vijana waliopo kati ya umri wa miaka 15-24 wako katika hatari kupatikana na magonjwa yanayosababishwa na ngono STI ikilinganishwa na watu wazima.
Mwaka 2016, vijana kati ya umri wa miaka 15-24 ambayo ni asilimia 62 walipatikana na ugonjwa wa klamidia , asilimia 50 na kisonono, asilimia 49 walikuwa na maambukizi katika sehemu za siri, huku asilimia 42 wakiwa na ugonjwa wa vidonda katika sehemu za siri
Wapenzi wa jinsia moja wako katika hatari ya kuambukizwa na magonjwa ya zinaa.
Ikilinganishwa na ngono kati ya wanawake ambao huonekana kuwa na hatari ya viwango vya chini, huku baadhi ya watu wakidhania kwamba wapenzi wa jinsia moja katika jinsia ya kike na wanawake wanaoshiriki katika mapenzi hayo na wanaume pamoja na wanawake hawako hatarini kupimwa magonjwa hayo ya zinaa.

Picha za orodha ya kinga wakati wa kufanya ngonoHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionPicha za orodha ya kinga wakati wa kufanya ngono

''Wakati nilipoanza kuwa na mpenzi katika miaka yangu ya ujana sikujua kwamba ngono salama ilikuwa muhimu kwa wapenzi wa jinsia moja hususan wasagaji''.
''Wapenzi wangu wa kwanza walikuwa pia hawajui kwa hivyo hatukutumia kinga yoyote'' .
''Lakini mpira huo wa kondomu wa mdomoni ulinifanya kugundua kwamba wasagaji pia ni muhimu kufanya ngono salama sawa na mtu yeyote yule''.
Kama mipira ya kondomu, mipira hiyo ya Dental Dams inaweza kuharibiwa na huuzwa katika pakiti.
Lakini kama kondomu sio rahisi kununua.
Zinaweza kupatikana katika maduka ya kuuza dawa na hununuliwa mitandaoni.
Kila mtu anaelewa kuhusu mipira ya kondomu na dawa za kuzuia mimba , Zote tulifunzwa shuleni.Lakini kondomu za mdomoni haziangaliliki.Ni wazi kwamba uingiliaji katika sehemu ya uke sio lazima ishirikishe uume katika wasagaji ama wanandoa.
Kuna hatari ya kusababisha maambukizi kupitia uingiliaji wa kidijitali hususan kama mtu ana kidonda ama mkwaruzo katika mkono na iwapo una kidonda na ulikigusa kabla ya kufanya ngono.

Labels: , ,

'Mazombi wa simu' kupigwa faini wakivuka barabara Honolulu

Honolulu
Honolulu limekuwa jiji la kwanza kubwa nchini Marekani kuifanya kuwa haramu kwa "mazombi wa simu" kuvuka barabara wakitumia au kutazama simu zao.
Serikali katika jiji hilo la Hawaii wameidhinisha sheria ya kutotekwa fikira ukitumia kivuko cha barabarani.
Hii ina maana kwamba ni marufuku hata kuitupia jicho skrini ya simu yako kwa muda mfupi ukivuka barabara.
Ukipatikana na kosa hilo utapigwa faini ya $15-$35 (£11-£27).
Ukirudia kosa hilo, unaweza kutozwa faini ya hadi $99 (£76), shirika la habari la KHNL Hawaii News Now limeripoti.
"Ni jambo la kimsingi, kwamba macho yako huwa hayatazami pale unapotakiwa kutazama na hilo huweka kila mtu hatarini. Kutazama chini kidogo hata muda mfupi kuangalia ujumbe kwenye simu, unaweza kukosa kuangalia barabara kwa sekunde tano," afisa wa polisi wa Honolulu James Shyer ameambia KHNL.
Wanaotembea kwa miguu hata hivyo bado wataweza kutumia simu zao wakitembea maeneo yaliyotengewa abiria barabarani.
Aidha, unaweza kusamehewa iwapo utatazama simu yako kupiga simu ya dharura, shirika la habari la NPR limesema.
Sheria hiyo iliidhinishwa kuwa sheria Julai lakini kulikuwa na miezi mitatu ya kuwahamasisha raia kabla ya kuanza kutekelezwa rasmi.
Wakati huo, meya Kirk Caldwell alisema Honolulu ni mji ambao ulikuwa na sifa mbaya ya watu wengi kugongwa na magari kwenye vivuko vya barabara - hasa watu wazima - kuliko mji wowote ule Marekani.
Miji mingine imekuwa pia ikifikiria kuchukua hatua sawa.
Kupiga simu ukivuka barabara bado ni haramuHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionKupiga simu ukivuka barabara bado ni haramu
Baraza la jiji la Toronto lilipiga kura kuomba serikali ya jimbo la Ontario kufanyia marekebisho sheria za trafiki kulifanya kuwa kosa mtu akitembea akiwa hisia zake zimetekwa.
Lakini serikali ya jimbo iliamua zaidi kuangazia kuhamasisha raia kuhusu hatari ya kufanya hivyo.
Afisa wa polisi wa Toronto Clint Stibbe aliambia CBC mnamo 25 Oktoba kwamba badala ya kupitisha sheria, abiria wanafaa kuwajibikia zaidi usalama wao

Labels: