Sunday 29 October 2017

Mamia ya wafuasi wa IS wakamatwa Uturuki

Polisi wa Uturuki wakiwa katika mazishi ya mmoja wa polisi mwenzo aliyeuawa na IS mwezi AgostiPolisi nchini Uturuki imewakamata mamia ya watu wanaodhaniwa kuwa wafuasi wa kikundi cha wanamgambo wa IS.
Raia wawili wa Azerbaijan na wengine 28 wa Syria, ni miongoni mwa waliokamatwa katika mji wa Mashariki wa Erzurum na mji wa Bursa uliopo Kaskazini Magharibi.
Wengine walikamatwa katika mji mkuu Ankara siku ya Jumamosi.
Mpiganaji wa IS aliwaua watu 39 katika ukumbi mmoja wa usiku uitwao Reina mjini Istanbul, na tukio hilo bado limeacha simanzi kubwa.

Labels:

1 Comments:

At 29 October 2017 at 16:37 , Blogger INJILI HALISI MINISTRY said...

Hilo nalo neno

 

Post a Comment

Subscribe to Post Comments [Atom]

<< Home